Salama Na Shikana Ep 17 | DYNAMITE Part 1
#YAHStoneTown #SalamaNa #PodCast
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL https://bit.ly/YahStoneTownSubs
Listen our Podcast on
Spotify Link https://spoti.fi/2Uxr6Cm
ApplePodcast Link https://apple.co/2Ou1bru
GooglePodcast Link https://bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
Audiomack Link https://bit.ly/YahStoneTownAudioMack
YouTube Link http://bit.ly/YoutubeSalamaNa
Mi na rafiki yangu huyu tumepishana zaidi ya miaka kumi na nne, wakati anazaliwa mimi nilikua nagombana na makondakta kupata nafasi kwenye chai maharagwe ya kutoka Buguruni kuelekea Posta. Ila kupishana kwetu kwa umri naamini ndo kunaufanya ushoga wetu uwe special zaidi, maana yeye akiwa ananikhadithia kinachokiki kwenye umri wake, nami nakua namuelezea challenges za unapozidi kukua na naamini hii inatufanya tuwe bora zaidi. Na ki ukweli mara nyingi yeye amekua shujaa wangu, maana kuna mengine mazito kwake yanakua mepesi tu na hunisaidia kuona mambo kwa picha tofauti. Kwa hilo namshukuru sana. Wakati mwengine wanasema umri sio kipimo cha busara, rafiki yangu huyu kupitia mengi, kwahiyo moyo wake wa ‘chuma’ unatusaidia wengi kwenye kuweza kupambana na dhurba mbali mbali.
Hapa sina haja hata ya kukuambia alipitia mitihani kiasi gani maana dunia nzima inajua, ila naweza tu kukuambia kwamba hakuna binti mwenye moyo wa utayari na ambae hana uwoga pale anapokua anasimamia lake kama Elizabeth Michael Kimemeta. Kwanza akiweka nia kwenye jambo lake lazima liwe... Atafunga, atakesha asali, ataweka akili na mawazo yake yote humo mpaka Mwenyezi Mungu amtimizie, nishashuhudia hilo sio mara moja wala mbili na naweza nikasema binafsi ameni inspire sana kwenye suala zima la funga na sala. Nani kamfundisha hayo? Kwa umri wake aliokua nao wakati matatizo mazito yalipomfika pengine usingedhani angekua binti wa dizaini hiyo. Miaka minne au mitano ambayo Alikutwa na yale matatizo ya kesi na mpaka akatumikia kifungo ni miaka ambayo ilimfaya akue sana. Ki imani na kiakili.
Kwenye kipindi hiki hakua bado tayari kuzungumzia usiku ule ulobadilisha maisha yake ila kaniahidi akiwa tayari basi atafiria kutushirikisha kwenye hayo maongezi ila inawezekana pia hiyo siku isifike, nna hisia hiyo ni kurasa ya kwenye kitabu ambayo amechagua kuiruka kwa sasa au pengine milele, na maamuzi hayo mimi na wenzangu tuliyaheshimu.
Sote tunakumbuka wakati anakua, kila kukicha yuko kwenye gazeti ila kwa sasa huyo si yule, amekua ki mwili, ki akili na hata ki sanaa pia. Mambo yake si ‘hadharani’ tena kama ilivyokua miaka ya nyuma. Sasa amekua influencer ambaye kampuni kubwa kadhaa zinamuamini yeye kuwatangazia biashara yao. Amekua Mama kwa mdogo wake Eric ambaye naye tumemuona akikua kwenye macho yetu. Mama kwa watoto wawili ambao amewakuta wakiwa wanaishi na mchumba wake nyumba moja.
Kwenye haya maongezi yetu tuligusia hilo la hao watoto, na watoto wengine, kazi, yeye kama binti ambae amekua akikutana na mawe mengi. Muonekano wake. Familia kwa upande wa Mama na Baba na mambo mengine kadhaa. Niko hapa kukutakia uangaliaji mwema wa kipindi hiki na yangu matumaini utavutiwa na jambo ambalo litakufanya ubadili maisha yako kwa uzuri zaidi. Tafadhali enjoy.
Love,
Salama.
Soundtrack Yeah by @MarcoChali https://www.youtube.com/watch?v=Cue1HB4fnLQ
Follow:
Twitter: http://twitter.com/YahStoneTown
Instagram: http://Instagram.com/YahStoneTown
Facebook: http://facebook.com/YahStoneTown
Видео Salama Na Shikana Ep 17 | DYNAMITE Part 1 канала YahStoneTown
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL https://bit.ly/YahStoneTownSubs
Listen our Podcast on
Spotify Link https://spoti.fi/2Uxr6Cm
ApplePodcast Link https://apple.co/2Ou1bru
GooglePodcast Link https://bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
Audiomack Link https://bit.ly/YahStoneTownAudioMack
YouTube Link http://bit.ly/YoutubeSalamaNa
Mi na rafiki yangu huyu tumepishana zaidi ya miaka kumi na nne, wakati anazaliwa mimi nilikua nagombana na makondakta kupata nafasi kwenye chai maharagwe ya kutoka Buguruni kuelekea Posta. Ila kupishana kwetu kwa umri naamini ndo kunaufanya ushoga wetu uwe special zaidi, maana yeye akiwa ananikhadithia kinachokiki kwenye umri wake, nami nakua namuelezea challenges za unapozidi kukua na naamini hii inatufanya tuwe bora zaidi. Na ki ukweli mara nyingi yeye amekua shujaa wangu, maana kuna mengine mazito kwake yanakua mepesi tu na hunisaidia kuona mambo kwa picha tofauti. Kwa hilo namshukuru sana. Wakati mwengine wanasema umri sio kipimo cha busara, rafiki yangu huyu kupitia mengi, kwahiyo moyo wake wa ‘chuma’ unatusaidia wengi kwenye kuweza kupambana na dhurba mbali mbali.
Hapa sina haja hata ya kukuambia alipitia mitihani kiasi gani maana dunia nzima inajua, ila naweza tu kukuambia kwamba hakuna binti mwenye moyo wa utayari na ambae hana uwoga pale anapokua anasimamia lake kama Elizabeth Michael Kimemeta. Kwanza akiweka nia kwenye jambo lake lazima liwe... Atafunga, atakesha asali, ataweka akili na mawazo yake yote humo mpaka Mwenyezi Mungu amtimizie, nishashuhudia hilo sio mara moja wala mbili na naweza nikasema binafsi ameni inspire sana kwenye suala zima la funga na sala. Nani kamfundisha hayo? Kwa umri wake aliokua nao wakati matatizo mazito yalipomfika pengine usingedhani angekua binti wa dizaini hiyo. Miaka minne au mitano ambayo Alikutwa na yale matatizo ya kesi na mpaka akatumikia kifungo ni miaka ambayo ilimfaya akue sana. Ki imani na kiakili.
Kwenye kipindi hiki hakua bado tayari kuzungumzia usiku ule ulobadilisha maisha yake ila kaniahidi akiwa tayari basi atafiria kutushirikisha kwenye hayo maongezi ila inawezekana pia hiyo siku isifike, nna hisia hiyo ni kurasa ya kwenye kitabu ambayo amechagua kuiruka kwa sasa au pengine milele, na maamuzi hayo mimi na wenzangu tuliyaheshimu.
Sote tunakumbuka wakati anakua, kila kukicha yuko kwenye gazeti ila kwa sasa huyo si yule, amekua ki mwili, ki akili na hata ki sanaa pia. Mambo yake si ‘hadharani’ tena kama ilivyokua miaka ya nyuma. Sasa amekua influencer ambaye kampuni kubwa kadhaa zinamuamini yeye kuwatangazia biashara yao. Amekua Mama kwa mdogo wake Eric ambaye naye tumemuona akikua kwenye macho yetu. Mama kwa watoto wawili ambao amewakuta wakiwa wanaishi na mchumba wake nyumba moja.
Kwenye haya maongezi yetu tuligusia hilo la hao watoto, na watoto wengine, kazi, yeye kama binti ambae amekua akikutana na mawe mengi. Muonekano wake. Familia kwa upande wa Mama na Baba na mambo mengine kadhaa. Niko hapa kukutakia uangaliaji mwema wa kipindi hiki na yangu matumaini utavutiwa na jambo ambalo litakufanya ubadili maisha yako kwa uzuri zaidi. Tafadhali enjoy.
Love,
Salama.
Soundtrack Yeah by @MarcoChali https://www.youtube.com/watch?v=Cue1HB4fnLQ
Follow:
Twitter: http://twitter.com/YahStoneTown
Instagram: http://Instagram.com/YahStoneTown
Facebook: http://facebook.com/YahStoneTown
Видео Salama Na Shikana Ep 17 | DYNAMITE Part 1 канала YahStoneTown
Показать
Комментарии отсутствуют
Информация о видео
Другие видео канала
Salama Na Shikana Ep 17 | DYNAMITE Part 2Salama Na NANDY Ep 53 | MNOGESHAJI PART 1Salama Na LAMATA SE6 EP 04 FULL SHOW |WATASWIRA PART 1| SendTip MPESA LIPA NO 5578460Salama Na VANNY BOY Ep 54 | NDAGHA PART 1Salama Na JK Ep 48| MSOGA UNO PART 1Salama Na TID SE6 EP07 FULL SHOW|NYOTA YAKO PART 1|SendTip MPESA LIPA NO 5578460Salama Na KING AliKiba SE6 Ep 03 FULL SHOW | DELIGHTFUL Part 1| SendTip MPESA LIPA NO 5578460Salama Na JOTI Ep 47 | SIMPLY SPECIAL PART 1Salama Na KAJALA Ep 35 | JERAHA LA MOYO Part 1LULU AFUNGUKA KUMKINGIA KIFUA WEMASEPETU/ALIVYOFULIA/HANA GARI/REEENGESalama Na Jokate Ep 3 | KAMISHNA Part 1Salama Na HENRY KULAYA SE6 EP13|MASTER PART 1|SendTip MPESA LIPA NO 5578460Salama Na Romy Jons Ep 14 | PLUG Part 1Salama Na Gigy Money Ep 12 | ZILE KHADITHI Part 1Salama Na Khadija Kopa Ep 9 | ALIYEPEWA KAPEWA Part 1Salama Na MwanaFA Ep 10 | KARAMA Part 1Salama Na Idris Ep 8 | TROOPER Part 1Lulu: Mimba / Sitaki TENA / Hamisa Mobeto / Nam-BLOCK! / Utoto Utoto!Salama Na RIYAMA Ep 32 | UTAKWENDA UTARUDI Part 1