Загрузка...

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko kusuasua MRADI UMEME CHALINZE- DODOMA

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesikitishwa kusuasua kwa MRADI WA UMEME WA CHALINZE- DODOMA huo aliouzindua Novemba 2024 kuwa nyuma kwa asilimia Saba

Asema Rais Samia alitoa agizo mradi usichezewe kutokana na umuhimu wake katika mikoa mbalimbali ikiwemo ya Magharibi

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amekagua mradi wa njia ya kusafirisha umeme ya msongo wa kilovolti 400 kutoka Chalinze hadi Zuzu Dodoma na kueleza kutoridhishwa kwake na utekelezaji wa mradi huo ambao ulipaswa kuwa umefikia asilimia 31 lakini kwa sasa umefikia asilimia 24 tangu kuzinduliwa kwake Novemba mwaka 2024.

Hali ya kusuasua kwa mradi imebainika wakati Dkt. Biteko akikagua mradi huo katika Kijiji cha Manchali wilayani Chamwino mkoani Dodoma tarehe 20 Agosti 2025 ambapo Dkt. Biteko amemuagiza mkandarasi kampuni ya TBEA ya China kuhakikisha kuwa anafidia muda wa kazi uliopotezwa wa asilimia Saba ili mradi ukamilike kwa wakati kutokana na umuhimu wake nchini.

Видео Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko kusuasua MRADI UMEME CHALINZE- DODOMA канала Kapo Digital
Яндекс.Метрика
Все заметки Новая заметка Страницу в заметки
Страницу в закладки Мои закладки
На информационно-развлекательном портале SALDA.WS применяются cookie-файлы. Нажимая кнопку Принять, вы подтверждаете свое согласие на их использование.
О CookiesНапомнить позжеПринять