UFUGAJI WA KUKU CHOTARA AINA YA SASSO KWA KUKU WA NYAMA
Kuku chotara wana faida nyingi sana katika kilimo cha biashara. Kuku chotara ni muunganiko au mchanganyiko wa aina mbili tofauti za kuku.
ufugaji wa kuku wa nyama
ufugaji wa kuku kuroiler
ufugaji wa kuku chotara pdf
ufugaji wa kuku chotara
ufugaji wa kuku jamii forum
ufugaji wa kuku wa kienyeji wenye tija
ufugaji wa kuku katika eneo dogo
ufugaji wa kuku 2021
Kuku hawa wana faida kadhaa kwako kama mjasiriamali mwenzetu:
Kuku hawa wanastahimili magonjwa. Hii inakusaidia kupunguza gharama za kuwatibu.
Kuku hawa wanataga mayai mengi tofauti na kuku wa kawaida wa kineyeji. Ukiwalisha vizuri wanaweza kutaga mpaka mayai 240 kwa mwaka, huu ukiwa ni wastani wa karibia yai 1 kwa siku.
Kuku hawa hukua kwa haraka na wana uwezo wa kufikia uzito wa kilogramu 3 katika muda wa miezi 3.
Unaweza kuwatumia hawa kuku kwa ajili ya kuuza kama nyama au kwa ajili ya kuzalisha mayai ya biashara.
Unataka Kuwafuga Kuku Hawa Kibiashara? Basi zingatia mambo makuu mawili: Usiwaache kuku wako kuatamia mayai. Kufanya hivi unawapotezea kuku wako muda wa kutaga. Kusanya mayai yako yatie kwenye mashine ya kutotorea vifaranga.
Au peleka kwa mfugaji mwenzako mwenye mashine (ambako utalipia gharama za kutotoresha kwa makubaliano).
Tengeneza chakula cha kuku wewe mwenyewe badala ya kununua. Kumbuka biashara yenye faida inaangalia gharama za uzalishaji dhidi ya bei ya kuuzia.
Hatua Za Ufugaji Wa Kuku Chotara Ili kufuga kuku chotara kwa ufanisi hakikisha unafanya mambo yafuatayo;
Andaa banda ambalo linafaa kwa matumizi ya ufugaji wa kuku.
Ukubwa wa banda uzingatie wingi wa kuku unaohitaji kufuga.
Banda lako linatakiwa liwe linapitisha hewa ya kutosha. Tafuta kuku wa kienyeji matetea (majike) na jogoo la kisasa aina yoyote kisha wachanganye katika banda moja. Unaweza kuanza na majike 2 na jogoo 1.
Hii itapelekea upate mayai chotara. Tumia mashine ya kutotoresha mayai ili kupata vifranga chotara. Kama haitawezekana kabisa tumia basi waache kuku waatamie mayai hayo.
Baada ya wiki tatu (siku 21) vifaranga watakuwa tayari kutotolewa kwa kutumia matetea ya kuku wa kienyeji au mashine ya kutotolesha vifaranga. Kwa muda wa wiki tatu hadi nne vifaranga wako wanahitaji joto la kutosha kwa ajili ya ukuaji na afya njema hivyo hakikisha unatumia kinengunengu kuwatunza (soma makala juu ya kinengungu hapo juu).
Vifaranga Wakiwa Tayari Chanjo Muhimu Inahitajika Ili Kuzuia Vifo Na Milipuko Ya Magonjwa Mbalimbali. Fuata hatua zifuatazo kuhakikisha vifaranga wako wanakua vyema: Siku ya kwanza hadi ya tatu tangu kutotolewa wapatie vifaranga glukosi na vitamini pamoja na chanjo za magonjwa ya Mahepe (Mareks disease) na Mdondo (Newcastle disease).
Siku ya 10 wapatie chanjo ya ugonjwa wa Gumboro. Siku ya 18 wapatie tena chanjo ya ugonwja wa Gumboro.
Siku ya 21 wapatie tena chanjo ya ugonjwa wa Mdondo. Wapatie pia chanjo ya ugonjwa wa ndui (fowl pox). Wiki ya 12 (siku ya 84) wapatie kuku wako chanjo ya ugonjwa wa homa ya matumbo (fowl typhoid).
ANGALIZO: Usichanganye maji ya chanjo na vitamini au glukosi. Chanjo ifanyike wakati wa jioni au asubuhi. Kamwe chanjo isifanyike wakati wa mchana. Hakikisha huchanji kuku wagonjwa bali wenye afya. Ukishachanganya chanjo kwenye maji, kuku wanywe maji hayo kwa muda wa masaa mawili tu baada ya hapo mwaga mchanganyiko huo na osha vyombo vya maji na uweke maji safi yaliyochanganywa na vitamini.
Tumia vyombo vya plastiki wakati wa kuchanganya na kuwapa kuku maji ya chanjo Wanyime kuku maji kwa masaa mawili kabla ya kuwapa maji ya chanjo. Weka kumbukumbu za chanjo uliyotumia ikiwemo toleo la chanjo (batch number). Vifaranga wapewe dawa ya kuzuia ugonjwa wa kuharisha damu (cocidiosis) kwa muda wa siku tatu mfululizo mara wafikishapo umri wa siku saba. Vifaranga wapewe dawa ya minyoo wafikishapo umri wa miezi miwili (siku 60) na baada ya hapo wapewe dawa ya minyoo kila baada ya miezi mitatu.
#mkulimasmart
#shambadarasa
Видео UFUGAJI WA KUKU CHOTARA AINA YA SASSO KWA KUKU WA NYAMA канала Shamba Darasa TV
ufugaji wa kuku wa nyama
ufugaji wa kuku kuroiler
ufugaji wa kuku chotara pdf
ufugaji wa kuku chotara
ufugaji wa kuku jamii forum
ufugaji wa kuku wa kienyeji wenye tija
ufugaji wa kuku katika eneo dogo
ufugaji wa kuku 2021
Kuku hawa wana faida kadhaa kwako kama mjasiriamali mwenzetu:
Kuku hawa wanastahimili magonjwa. Hii inakusaidia kupunguza gharama za kuwatibu.
Kuku hawa wanataga mayai mengi tofauti na kuku wa kawaida wa kineyeji. Ukiwalisha vizuri wanaweza kutaga mpaka mayai 240 kwa mwaka, huu ukiwa ni wastani wa karibia yai 1 kwa siku.
Kuku hawa hukua kwa haraka na wana uwezo wa kufikia uzito wa kilogramu 3 katika muda wa miezi 3.
Unaweza kuwatumia hawa kuku kwa ajili ya kuuza kama nyama au kwa ajili ya kuzalisha mayai ya biashara.
Unataka Kuwafuga Kuku Hawa Kibiashara? Basi zingatia mambo makuu mawili: Usiwaache kuku wako kuatamia mayai. Kufanya hivi unawapotezea kuku wako muda wa kutaga. Kusanya mayai yako yatie kwenye mashine ya kutotorea vifaranga.
Au peleka kwa mfugaji mwenzako mwenye mashine (ambako utalipia gharama za kutotoresha kwa makubaliano).
Tengeneza chakula cha kuku wewe mwenyewe badala ya kununua. Kumbuka biashara yenye faida inaangalia gharama za uzalishaji dhidi ya bei ya kuuzia.
Hatua Za Ufugaji Wa Kuku Chotara Ili kufuga kuku chotara kwa ufanisi hakikisha unafanya mambo yafuatayo;
Andaa banda ambalo linafaa kwa matumizi ya ufugaji wa kuku.
Ukubwa wa banda uzingatie wingi wa kuku unaohitaji kufuga.
Banda lako linatakiwa liwe linapitisha hewa ya kutosha. Tafuta kuku wa kienyeji matetea (majike) na jogoo la kisasa aina yoyote kisha wachanganye katika banda moja. Unaweza kuanza na majike 2 na jogoo 1.
Hii itapelekea upate mayai chotara. Tumia mashine ya kutotoresha mayai ili kupata vifranga chotara. Kama haitawezekana kabisa tumia basi waache kuku waatamie mayai hayo.
Baada ya wiki tatu (siku 21) vifaranga watakuwa tayari kutotolewa kwa kutumia matetea ya kuku wa kienyeji au mashine ya kutotolesha vifaranga. Kwa muda wa wiki tatu hadi nne vifaranga wako wanahitaji joto la kutosha kwa ajili ya ukuaji na afya njema hivyo hakikisha unatumia kinengunengu kuwatunza (soma makala juu ya kinengungu hapo juu).
Vifaranga Wakiwa Tayari Chanjo Muhimu Inahitajika Ili Kuzuia Vifo Na Milipuko Ya Magonjwa Mbalimbali. Fuata hatua zifuatazo kuhakikisha vifaranga wako wanakua vyema: Siku ya kwanza hadi ya tatu tangu kutotolewa wapatie vifaranga glukosi na vitamini pamoja na chanjo za magonjwa ya Mahepe (Mareks disease) na Mdondo (Newcastle disease).
Siku ya 10 wapatie chanjo ya ugonjwa wa Gumboro. Siku ya 18 wapatie tena chanjo ya ugonwja wa Gumboro.
Siku ya 21 wapatie tena chanjo ya ugonjwa wa Mdondo. Wapatie pia chanjo ya ugonjwa wa ndui (fowl pox). Wiki ya 12 (siku ya 84) wapatie kuku wako chanjo ya ugonjwa wa homa ya matumbo (fowl typhoid).
ANGALIZO: Usichanganye maji ya chanjo na vitamini au glukosi. Chanjo ifanyike wakati wa jioni au asubuhi. Kamwe chanjo isifanyike wakati wa mchana. Hakikisha huchanji kuku wagonjwa bali wenye afya. Ukishachanganya chanjo kwenye maji, kuku wanywe maji hayo kwa muda wa masaa mawili tu baada ya hapo mwaga mchanganyiko huo na osha vyombo vya maji na uweke maji safi yaliyochanganywa na vitamini.
Tumia vyombo vya plastiki wakati wa kuchanganya na kuwapa kuku maji ya chanjo Wanyime kuku maji kwa masaa mawili kabla ya kuwapa maji ya chanjo. Weka kumbukumbu za chanjo uliyotumia ikiwemo toleo la chanjo (batch number). Vifaranga wapewe dawa ya kuzuia ugonjwa wa kuharisha damu (cocidiosis) kwa muda wa siku tatu mfululizo mara wafikishapo umri wa siku saba. Vifaranga wapewe dawa ya minyoo wafikishapo umri wa miezi miwili (siku 60) na baada ya hapo wapewe dawa ya minyoo kila baada ya miezi mitatu.
#mkulimasmart
#shambadarasa
Видео UFUGAJI WA KUKU CHOTARA AINA YA SASSO KWA KUKU WA NYAMA канала Shamba Darasa TV
Показать
Комментарии отсутствуют
Информация о видео
Другие видео канала
NILIANZA KUFUGA KUKU CHINI Leo Natumia LOCAL CAGES KUFUGIA KUKUUFUGAJI WA KUKU 2023 |TUMIA NJIA MPYA ZA KEJI/LOCAL CAGES KUFUGIA KUKU|KILIMO CHA MBOGAMBOGA,Karibu shamba la MTIMBI'S FARM DODOMAUTARATIBU WA KUJENGEWA LOCAL CAGESLOCAL H TYPE CAGES #mkulimasmart #shambadarasaKILIMO CHA NYANYA MSIMU WA KIANGAZI Tumia mbegu YA Jarrah F1BANDA LA KUKU LA GHOROFA uongeza eneo la kufuga kukuFAIDA ZA KUTUMIA BATTERY CAGES ZA MKULIMA SMART #chickencage #mkulimasmart #farming #shambadarasaMFUGAJI WA KUKU TUMIA LOCAL KEJI UTAJIRIKEUFUGAJI WA KUKU WA KISASA. |TUMIA LOCAL CAGES KUFUGIA KUKU|KUKU 1200LOCAL CAGE YA KUFUGA KUKU 1000BATA BUKINI AINA YA AFRICAN GOOSE WANAUZWALOCAL CAGES ZA MKULIMA SMART #mkulimasmartUFUGAJI WA SUNGURA KIBIASHARA NA SOKO LA SUNGURA TANZANIA:Fursa ya nyama ya sunguraMAFUNZO YA KILIMO CHA MATANGO KUTOKA THE YOUNG WORLD FEEDERS 2022KUKU WA MAYAI WANATAGA ASILIMIA 90NJOO TUKUFUNDISHE KUFUGA KUKU.UFUGAJI WA KUKU 1200 TUUFUGAJI WA BATA BUKINI |AFRICAN GOOSE WANAUZWA|KILIMO CHA NYANYA 2022;Zijue changamoto zinazokabili wakulima wa nyanya Tanzania.