Загрузка...

🕌 RAIS MWINYI AFUNGUA MSIKITI MPYA NUNGWI! ATOA WITO MZITO KWA WAUMINI

Rais Dķt, Mwinyi ameyasema hayo leo Tarehe 24 April 2026 alipojumuika na Waumini wa Dini ya Kiislamu katika Sala ya Ijumaa ilioyambatana na Ufunguzi wa Msikiti Mpya wa Jamaa Nour uliopo Boshowa Nungwi, Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Ameeleza kuwa Zipo Changamoto nyingi katika jamii zinazohitaji kupatiwa Ufumbuzi husani zile wanazokabiliana Nazo Watu wa Makundi Maalumu ya Wajane ,Wazee wasiojiweza na Watoto,Wqtu wenye Ulemavu na Mayatima .

Aidha Alhaji Dkt Mwinyi amesema Waumini wqna Wajibu Mkubwa wa kuitumia Misikiti kujifunza na Kusomeahana Dini hususani kwa Watoto ili wqijue vema Dini yao pamoja na kusali kwa bidii na kumcha Mwenyezi Mungu kwani ndio Sababu kuu ya kujengwa Misikiti mikubwa na Mizuri katika Maeneo mbalimbali.

Alhaji Dkt, Mwinyi amewahimiza Waumini wa Dini ya Kiislamu kuutunza Msikiti huo Mpya ili ubaki katika haiba na Mazingira bora wakati wote kwa kutafuta Utaratibu mzuri wa kuchangia pamoja na Kuwatunza Maimamu na Walimu wa Madrasa pamoja na kumshukuru Mfadhili wa huo Msikiti kwa Uamuzi wake .
Akiwasilisha Salamu za Waumini wa Msikiti huo Sheikh Haji Kombo Khamis amesema Ujenzi wa Msikiti huo ni Msaada mkubwa kwa Waumini wa Eneo hilo kwani umeondoa tatizo la muda mrefu la kusali katika Msikiti mdogo usiokidhi nafasi kwa Waumini na kumshukuru Mfadhili wa Msikiti huo .

Видео 🕌 RAIS MWINYI AFUNGUA MSIKITI MPYA NUNGWI! ATOA WITO MZITO KWA WAUMINI канала Tifu Tv
Яндекс.Метрика
Все заметки Новая заметка Страницу в заметки
Страницу в закладки Мои закладки
На информационно-развлекательном портале SALDA.WS применяются cookie-файлы. Нажимая кнопку Принять, вы подтверждаете свое согласие на их использование.
О CookiesНапомнить позжеПринять